Saturday, June 14, 2014

Mitaa na Koo

                           
Luhira ni kitongoji kilichopo katika kata ya seed farm kwenye halmashauri ya Manispaa ya Songea, kilometa nne mashariki kwenye barabara iendayo Tunduru. Ni eneo lenye umuhimu wa aina yake katika ustawi wa mji wa Songea kutokana na kuwa na vitu kadhaa, baadhi yake ikiwa ni mito miwili ya kudumu yenye maji safi wakati wote wa mwaka, mto fataki na mto luhira ambao kwa sasa ni mto wa hifadhi unaotumika kwa mradi mkubwa wa usambazaji maji. Pia Luhira kuna shule kongwe ya sekondari ya Songea Boys High School ambayo kwa kweli ni miongoni mwa taasisi kubwa kabisa za elimu za umma nchini. Pia kuna mlima Unangwa.

Luhira ni kubwa, na imegawanyika katika mitaa kadhaa, ambayo imepewa majina kulingana koo zilizokuwa zikiishi maeneo hayo tangu zamani.

                                 i.            Kwa Mchawa
                               ii.            Kwa Mangoma
                              iii.            Kwa Mkeso
                             iv.            Kwa Mngwale
                               v.            Kwa Kipande
                             vi.            Kwa Msabata
                            vii.            Kwa Kapolo
                          viii.            Kwa Koplo
                   ix.        Kwa Rupia
Jamii ya wanaluhira ni jamii mchanganyiko yenye watu wa makabila tofauti. Mitaa yetu ina majina ya koo si kwa maana ya kuwa eneo hilo linakaliwa na wanaukoo wenye jina hilo pekee, la. Ni kwa sababu hapo zamani eneo fulani lilikuwa likimilikiwa na watu wa ukoo fulani wakiishi na kuendesha shughuli zao nyingine za uzalishaji mali.

3 comments:

  1. Your post is very informative. Did you know that women can buy Abortion Pills online USA to maintain privacy and safety during difficult times? Keep spreading awareness about accessible healthcare options.

    ReplyDelete
  2. Great insights! Many women face challenges accessing care, which is why websites like abortionpillrx247.com let you buy Abortion pills online with 24/7 support.

    ReplyDelete